Sunday, 20 April 2008

Chenge mbona anatuchengua!


Chenge ni bilionea wa kutupwa ambaye kwake shilingi Bilioni moja anayodaiwa kuificha huko Marekani ni sawa na "vijisenti" vichache. Hivi tatizo letu liko wapi? Je yawezekena kuwa chenge ni dalili tu ya tatizo? Je eye ni kiongozi pekee wa TAnzania ambaye amewekeza mabilioni ya shilingi kwenye akaunti za kigeni? Je ajiuzulu au na yeye anaweza akalia kuwa amefanywa "Bangusilo" wa rada!?
Hata hivyo, habari zilizopatiakana hivi punde zinaeleza kuwa tayari mheshimiwa Chenge amejiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu.


Habari hii ni kwa mujibu wa Mwanakijiji anayepatikana katika mtandao wa http://mwanakijiji.podomatic.com/

No comments: