Wednesday 30 April 2008

BONANZA LA VYUO VIKUU MJINI MOROGORO




Picha ya juu inawaonesha wachezaji wa MUM wakijiandaa kuingia katika ngwe ya pili ya mchezo wa fainali dhidi ya Chuo Kikuu cha Mzumbe ambapo timu hiyo ilichapwa mabao 2-1 katika uwanja wa Jamhuri.
Picha ya pili inamuonesha mshambuliaji hatari wa timu ya mpira wa pete ya MUM akiwa amepumzika mara baada ya kuiwezesha timu yake kutwaa kombe la Bonanza.
Picha ya chini inawaonesha wachezaji wa timu ya MUM wakiwa katika mapumziko wakati wa mchezo wa fainali dhidi ya Mzumbe.

Duuuh! hapo tunaenda sawa


Kikwete na Tshivangirai

Rais wa Jamhuri ya Muungano ambaye ni Mwenyekiti wa AU Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na kiongozi wa chama cha upinzani nchini Zimbabwe MDC Bw. Morgan Tshivangirai walipokutana nchini Ethiopia.

Rostam kachukua uamuzi sahihi au vitisho?


Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz (CCM) ameamua kulishtaki gazeti la Mwanahalisi na wakati huo huo kulitishia gazeti la Raia Mwema kuwa atalifungulia mashtaka endapo halitaomba radhi kwa mojawapo ya makala zake.

Bw. Rostam anakuwa kiongozi wa kwanza ambaye amekuwa akitajwa na vyombo vya habari kuhusu ufisadi aliyeamua kwenda mahakamani. Kwa namna ya pekee hli linaashiria mambo kadhaa.

Kwanza, endapo mahakama itaridhia maombi yake basi masuala ya Richmond na Rostam yanaweza yasitajwe kwenye sentensi moja kwani kesi itakuwa mahakamani . Huu ni mchakato wa Kisheria na vyombo husika vitatakiwa kuheshimu, ingawa hilo halitufungi sisi wengine kutolea maoni.

Pili, kujaribu kunyamazisha vyombo hivyo vya habari endapo kutakubaliwa na mahakama basi kutazuia habari mpya kuweza kuchapwa na gazeti hilo . Hata hivyo, sisi wengine tutaweza kuendelea kutolea maoni.

Jambo la tatu ni kuwa Bw. Rostam amefanya jambo la maana kwa kuamua kwenda mahakamani hasa kwa vile anaamini haki yake inatishiwa na jina lake kuchafuliwa. Hivyo, uamuzi wake ni mfano wa kuigwa kwa wengine ambao wanahisi kuonewa au kutotendewa haki ili watumie vyombo vya sheria kutafuta haki hiyo badala ya kukimbilia kwenye TV au radio kujisafisha.
Hata hivyo, kama kesi hii itanedelea au itaishia pembeni hatuna uhakika. Hata hivyo vyanzo vyangu vya karibu na MwanaHalisi vimenihakikishia kuwa hawana mpango wa ku "back down" na wanaendelea kufanyia kazi taarifa nyngine kuhusu Rostam na Richmond. Sisi wengine yetu ni macho tu.

Je wadaiwa wengine na wale wanaotajwa kwenye tuhuma za ufisadi na wenyewe waende mahakamani? Je ndiyo njia pekee ya wao kujisafisha? Kwanini wale wengine waliotishia kwenda mahakamani hawakwenda?

Habari hii ni kwa mujibu wa Mwanakijiji
http://mwanakijiji.podomatic.com/

Sunday 27 April 2008

The Comedy

Hili ni kundi la vichekesho la the Comedy linalotamba katika kituo cha Televisheni cha East Africa.