Saturday 15 March 2008

Vipaji

Watoto wakionesha uwezo wao. Vijana kama hawa wanatakiwa kuendelezwa ili kukuza soka nchini.

Wataalamu

Wanafunzi wa Mawasiliano ya Umma mwaka wa tatu, Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro wakifuatilia Mhadhara wa Shaka Ssali Mtangazaji wa VOA (hayupo pichani)

Shaka Ssali

Mtangazaji wa Sauti ya Amerika (VOA) alipotembelea Chuo Kikuu Cha Waislamu Morogoro, mwishoni mwa mwaka 2007. Hapa anaongea na vijana wa Mawasiliano ya Umma mwaka wa tatu (hawapo pichani)

Maximo

Kutoka kushoto ni Mohammed Msemo, Kocha wa Taifa Stars Maximo na Mimi. Hapa tukiwa uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Matamu

Dr. Shukuru Kawambwa alipokuwa Waziri wa Maji. Hapa yupo kijiji cha Nyakabindi Mkoa wa Shinyanga akinywa maji ya Kisima alichokizindua.

'Birthday'

Mtoto Kauthar, hapa anatimiza miaka mitano. Kulea sio mchezo. Akiwa London wanakoishi wazazi wake.

Mhogo


Maonyesho ya Nanenane 2007, Mkoani Morogoro. Hii ni Mbegu kutoka Mkoa wa Shinyanga.

Papai

Hapa ni Morogoro kwenye maonesho ya Nanenane 2007. Pichani ni kijana wa Muslim University of Morogoro Bashir Salum akijipima nguvu kwa kunyanyua Papai. Haya mambo yanawezekana kama wakulima wetu wakiwezeshwa.

Maji

Mbunge wa Same Mashariki (CCM) Mheshimiwa Anne Kilango Malecela akimtwisha mtoto ndoo ya Maji. Anaye 'pampu' maji ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa Zanzibar Bi. Castico. Miradi kama hii ni muhimu kwa mustakbali wa wananchi wetu haswa wa vijijini. Hapa ni Kijiji cha Kihurio Same Mkoa wa Kilimanjaro.

Ugali huu

Nyumbani ni nyumbani. Pichani ni ndugu wakipata ugali. Picha hii niliinasa nilipotembelea Kijiji cha Dule Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga.

Ajali

Mambo ya kawaida kwenye nchi za ulimwengu wa Tatu. Niliinasa hii safarini Mtwara